
Andre Villas Boas.
Akiwa jicho moja ametumbulia mechi ya Jumapili, Villas-Boas alimpumzisha nahodha John Terry na Frank Lampard alikuwa katika benchi la wachezaji wa akiba.
Villas-Boas amesema: "Tutakwenda kujaribu kushinda. Itakuwa mechi nzuri sana nyakati hizi ligi ikiwa katika hatua za mwanzo."
Ameongeza: "Tunakabiliana na United pengine katika kipindi kizuri zaidi kilichojaa motisha, vipaji na mbinu nyingi za kupendeza za uchezaji.
Chelsea walionekana kun'gara muda mwingi wa mchezo dhidi ya timu hiyo ya Ujerumani, huku mshambuliaji anayechezea pia timu ya Taifa ya England chini ya umri wa miaka 21 Daniel Sturridge akiwa anaisumbua sana ngome ya Bayer Leverkusen kabla Luiz kufunga bao katika dakika ya 67 na Mata akaihakikishia ushindi kwa kupachika bao la pili zikiwa zimesalia dakika chache kabla mpira haujamalizika.
Matokeo hayo yamemfurahisha sana Villas-Boas, ambaye alisema: "Tulipata nafasi nyingi katika mchezo huo na tulistahili kushinda.
No comments:
Post a Comment